Kanisa anglikana Dayosisi ya Dar es salaam

Historia yetu

Kujua historia ya dayosisi yetu ya Dar es salaam

Kanzi data

Kupata huduma mbalimbali kwa njia ya kieletroniki

Sinodi

Kupata taarifa mbalimbali za sinodi iliyopita

Karibu Kanisa Anglikana, Dayosisi ya Dar-es-salaam

“Nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuziona kazi zenu njema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.”
Mathayo 5:16

Tukiwa tumejikita mizizi katika imani na huduma za kiroho na kijamii, Kanisa Anglikana dayosisi ya Dar es Salaam ni jumuiya ya Kikristo inayolenga kumtangaza Kristo, kukuza imani ya  waumini, na kubadilisha maisha ya jamii yetu kwa ujumla kwa kuzingatia misingi ya  upendo na huruma.

Kupitia ibada zetu, na huduma za kijamii kama elimu, afya, na huduma nyinginezo za kijamii, dayosisi yetu inalenga kumtukuza Mungu na kuwahudumia watu wake kwa uaminifu na moyo wa upendo.

Ujumbe kutoka kwa Askofu

Neema na amani viwe pamoja nanyi katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo.”
Karibu katika familia yetu ya Dayosisi. Tumeitwa kuwa nuru ya Kristo katika jiji hili — kuhudumu kwa uaminifu, kufundisha kwa kweli, na kuishi kwa upendo. Tunapokua pamoja katika imani, na tuendelee kuimarisha ushirika na kuleta mabadiliko chanya katika jamii zetu kwa utukufu wa Mungu.

✝️Ni sisi Jackson Sostenes Jackson

Askofu wa Dayosisi ya Dar es Salaam

Kuhusu Dayosisi

“Nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuziona kazi zenu njema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.”
— Mathayo 5:16

 Kanisa Anglikana dayosisi ya Dar es Salaam ni mojawapo ya dayosisi muhimu ndani ya Kanisa  Anglikana Tanzania. Ina mitaa na vigango yenye uhai vilivyomo ndani ya achidikonari tisa, ambazo ni Ubungo, Kinondoni, Ilala, Temeke, Kibaha, Upanga, Bagamoyo, Ukonga na Kigamboni. Makanisa haya  yanayoongozwa na wachungaji, mashemasi,wainjilisti, na viongozi mbalimbali ambao ni sehemu ya  waumini.

Idara zetu

Dayosisi yetu inaendeshwa na idara mbalimbali zinazofanya majukumu ya kila siku ya kiutawala , kama fedha, uinjilisti, ardhi, habari na mawasiliano.

Taasisi Zetu

Dayosisi yetu ina miliki taasisi kadhaa zinazotoa huduma za kijamii kwa watu wote, huduma hizi ni pamoja na , afya, elimu, pamoja na huduma za malazi.

Vikundi Vyetu

Dayosisi yetu in vikundi mbalimbali, vinavyochagiza uenezaji wa injili pamoja na huduma za kijamii, vikundi hivyo ni UMAKI, UBAKI pamojana TAYO.

Taarifa fupi kuhusu dayosisi yetu kwa kupitia namba

Mapadre
Wainjilist & walimu wa dini
Walimu wa Shule ya jumapili
Waumini
+
Achidikonari
Mitaa
Vigango
Jumuia
+

Habari na Matukio

“Njoni tumwabudu, tupige magoti mbele za Bwana Mtengenezaji wetu.” 

Zaburi 95:6

Pata taarifa za matukio mbalimbali yanayotokea ndani ya dayosisi, ikiwemo ibada kwenye mitaa na vigango mbalimbali,  ziara mbalimbali za Askofu, ziara za kichungaji, na huduma za jamii kupitia chanel yetu ya Anglican Tv.

ili kufuatilia vipindi na ibada mbalimbali tafadhali bofya kitufe hapo chini

Ibada zetu

“Njoni tumwabudu, tupige magoti mbele za Bwana Mtengenezaji wetu.” – Zaburi 95:6

Ilipo Mitaa yetu

Ungana nasi kila Jumapili kwenye ibada kwa lugha ya  Kiingereza kwenye baadhi ya mitaa yetu na  ibada kwa lugha ya Kiswahili katika mitaa,na vigango vyetu vyote.

Pia tuna ibada za katikati ya juma, pamoja na ibada za jumuiya kila siku ya jumamosi, kwenye mitaa na vigango husika.

Wasiliana nasi

Kupata huduma , taarifa na msaada wa kiroho na kiutendaji kutoka dayosisi tafadhali wasiliana nasi  au tutembelee ofisini

Makao makuu

Nyumba no. 35
Mtaa wa Arusha/Moshi
Ilala, Dar es salaam

Tupigie

+255 745 960 998
+255 760 960 883
+255 716 959 995

Tuandikie

info@anglicandar.org
actdiosm@gmail.com
habari@anglicandar.org

Waliotutembelea

  • Today's visitors:0
  • Today's page views 0
  • Total visitors 188
  • Total page views 196