Kanzi Data ya Dayosisi
Taarifa kwa maendeleo endelevu
Karibu kwenye mfumo wa ukusanyaji na utunzaji wa taarifa mbalimbali za dayosisi. Mfumo huu unaunganisha kumbukumbu zote za dayosisi katika sehemu moja, kuhakikisha upatikanaji rahisi na usahihi wa taarifa . Mfumo huu unauwezo wa kutoa huduma mbalimbali zinazopatikana kwenye ofisi za dayosisi kwa njia ya kieletroniki, ikiwemo kufanya yafuatayo
Kufanya Usajili
Mfumo huu unawezesha usajiri wa Mitaa, makasisi, wafanyakazi, waumini, idara, pamoja na rasilimali za dayosisi ili kuwezesha mawasiliano, usimamizi na mgawanyo wa rasilimali kwa ufanisi ili kuongeza ushiriki na matumizi bora ya rasilimali za dayosisi.
Kutunza kumbukumbu
uhifadhi kumbukumbu za kina na zilizopangwa vizuri za Mitaa, makasisi, wafanyakazi, waumini, idara mbalimbali pamoja na rasilimali za dayosisi ili kuwezesha mawasiliano na usimamizi usio na vikwazo, ili kuhakikisha ufuatiliaji kamili na upatikanaji rahisi wa taarifa.
Kutengeneza ripoti
Mfumo huu unatengeneza ripoti zenye taarifa muhimu za rasilimali watu, fedha, na mali, zinazowasaidia viongozi wa dayosisi kufuatilia utendaji na kupanga rasilimali kwa ufanisi ili kusaidia maamuzi sahihi na kuimarisha uwazi katika dayosisi nzima.
Takwimu za Dayosisi
Pata taarifa fupi kuhusu dayosisi yetu kwa kupitia takwimu hizi
Fomu za Usajili
Huduma Kiganjani mwako
Chagua fomu husika hapo chini ili uweze kusajiliwa na kupata huduma mbalimbali zitolewazo na dayosisi kwa njia ya mtandao.
Wasiliana nasi
Kupata huduma , taarifa na msaada wa kiroho na kiutendaji kutoka dayosisi tafadhali wasiliana nasi au tutembelee ofisini
Nyumba no. 35
Mtaa wa Arusha/Moshi
Ilala, Dar es salaam
+255 745 960 998
+255 760 960 883
+255 716 959 995
info@anglicandar.org
actdiosm@gmail.com
habari@anglicandar.org
- Today's visitors:10
- Today's page views 10
- Total visitors 271
- Total page views 283
Ilipo Mitaa yetu
Ungana nasi kila Jumapili kwenye ibada kwa lugha ya Kiingereza kwenye baadhi ya mitaa yetu na ibada kwa lugha ya Kiswahili katika mitaa,na vigango vyetu vyote.
Pia tuna ibada za katikati ya juma, pamoja na ibada za jumuiya kila siku ya jumamosi, kwenye mitaa na vigango husika.